Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Serikali yamshika mkono Babu Seya hadi studio
Michezo

Serikali yamshika mkono Babu Seya hadi studio

Familia ya Babu Seya wakiwa Ikulu kumshukuru Rais wa John Magufuli
Spread the love

SERIKALI imetangaza kuwabeba wasanii waliokuwa wamefungwa jela maisha ambao Desemba 9, 2017 walipewa msamaha na Rais John Magufuli ili kuinua vipaji vyao. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza leo amembeba Nguza Viking aliyekuwa amehukumiwa maisha kwa kosa la ubakaji na kutembelea studio za Wanene Entertainment zilizopo Mwenge Dar es Salaaam

Babu Seya aliongozana na mwanaye Johnson Nguza ‘ Papii Kocha.

Akizungumza leo na wanahabari Shonza amesema wizara yake ambayo ina dhamana na tasnia ya muziki imeamua kwa dhati kuwasaidia wasanii hao.

“Sisi kama wizara tumeamua kuendeleza vipaji vya wasanii hawa ambao sisi ndio walezi wao, hivyo nimewasiliana na uongozi wa Wanene ambao wamekubali kushirikiana na sisi lengo ni kuhakikisha ubora wa hawa wasanii unarejea na wanafanya kazi” amesema Shonza.

Wasanii hao walipelekwa katika studio hizo na Shonza na kupokelewa na mmiliki wa Wanene, Dash ambapo walifanya mazungumzo ya pamoja yaliyolenga kurekodi nyimbo kwa wasanii hao na kusaidiwa kurudisha vipaji vyao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!