SERIKALI imetangaza kuwabeba wasanii waliokuwa wamefungwa jela maisha ambao Desemba 9, 2017 walipewa msamaha na Rais John Magufuli ili kuinua vipaji vyao. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza leo amembeba Nguza Viking aliyekuwa amehukumiwa maisha kwa kosa la ubakaji na kutembelea studio za Wanene Entertainment zilizopo Mwenge Dar es Salaaam
Babu Seya aliongozana na mwanaye Johnson Nguza ‘ Papii Kocha.
Akizungumza leo na wanahabari Shonza amesema wizara yake ambayo ina dhamana na tasnia ya muziki imeamua kwa dhati kuwasaidia wasanii hao.
“Sisi kama wizara tumeamua kuendeleza vipaji vya wasanii hawa ambao sisi ndio walezi wao, hivyo nimewasiliana na uongozi wa Wanene ambao wamekubali kushirikiana na sisi lengo ni kuhakikisha ubora wa hawa wasanii unarejea na wanafanya kazi” amesema Shonza.
Wasanii hao walipelekwa katika studio hizo na Shonza na kupokelewa na mmiliki wa Wanene, Dash ambapo walifanya mazungumzo ya pamoja yaliyolenga kurekodi nyimbo kwa wasanii hao na kusaidiwa kurudisha vipaji vyao.
Leave a comment