Sunday , 3 December 2023
Home Kitengo Michezo Serikali yamshika mkono Babu Seya hadi studio
Michezo

Serikali yamshika mkono Babu Seya hadi studio

Familia ya Babu Seya wakiwa Ikulu kumshukuru Rais wa John Magufuli
Spread the love

SERIKALI imetangaza kuwabeba wasanii waliokuwa wamefungwa jela maisha ambao Desemba 9, 2017 walipewa msamaha na Rais John Magufuli ili kuinua vipaji vyao. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza leo amembeba Nguza Viking aliyekuwa amehukumiwa maisha kwa kosa la ubakaji na kutembelea studio za Wanene Entertainment zilizopo Mwenge Dar es Salaaam

Babu Seya aliongozana na mwanaye Johnson Nguza ‘ Papii Kocha.

Akizungumza leo na wanahabari Shonza amesema wizara yake ambayo ina dhamana na tasnia ya muziki imeamua kwa dhati kuwasaidia wasanii hao.

“Sisi kama wizara tumeamua kuendeleza vipaji vya wasanii hawa ambao sisi ndio walezi wao, hivyo nimewasiliana na uongozi wa Wanene ambao wamekubali kushirikiana na sisi lengo ni kuhakikisha ubora wa hawa wasanii unarejea na wanafanya kazi” amesema Shonza.

Wasanii hao walipelekwa katika studio hizo na Shonza na kupokelewa na mmiliki wa Wanene, Dash ambapo walifanya mazungumzo ya pamoja yaliyolenga kurekodi nyimbo kwa wasanii hao na kusaidiwa kurudisha vipaji vyao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

error: Content is protected !!