Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Tangulizi Serikali yatangaza bomoa bomoa Dar-Arusha
Tangulizi

Serikali yatangaza bomoa bomoa Dar-Arusha

Mkurugenzi wa  TRL,  Masanja  Kadogosa
Spread the love

KAMPUNI ya Reli (TRL), imetangaza kubomoa nyumba zote zilizojengwa kando kando mwa reli inayotoka Dar es salaam, Moshi  hadi jijini Arusha, anaandika Angela Willium.

Kadhalika, TRL imetangaza kuanza kuifanyia ukarabati mkubwa reli hiyo ili ianze kutumika kusafirishisha mizigo kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa  TRL,  Majanja  Kadogosa katika ziara  ya   Naibu Waziri wa Ujenzi  ,Uchukuzi na Mawasiliano,  Atashasta Nditiye amesema  baadhi ya nyumba zilizopo kwenye eneo la reli wameshaziwekea alama ya X.

Amesema alama ya X imeweka katika mikoa ya Morogoro na Dodoma ambapo inajengwa reli kubwa ambayo itapitisha Treni ya kutumia umeme.

“Tunawaomba wananchi waliovamia maeneo ya reli kuondoka mapema kabla ya kuanza zoezi la bomoa bomoa  nyumba zao tumeshaziweka alama ya X”.

Kadogosa amesema wamekuwa na changamoto ya ubovu wa reli pamoja na upungufu wa wafanyakazi na kuomba waboreshewe maslai ya watumishi.

Kuhusu ujenzi wa reli ya mikoa ya Kaskazini, alisema wameshaanza na kwamba hivi sasa wamefika Mombo na itachukua miezi  7 hadi 8  kukamilika.

Kwa upande wake, Nditiye amesema kutokana na changamoto iliyopo ya kuwaondoa wananchi waliovamia eneo la reli aliwaomba kupisha na kwamba ambao wataingiliwa na reli watalipwa fidia.

Ukarababti wa reli ya Moshi hadi Arusha  utakamilika ifikapo mwaka 2019 na lengo la ujenzi huo ni kukuza uchumi wa Tanzania na kutoa huduma kwa wananchi kwani gari moshi itabeba mizigo na nyingine  itachukua abiria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

Habari za SiasaTangulizi

Samia ataja miradi ambayo Tanzania inashirikiana na IDA

Spread the loveRais wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan leo Jumatatu amehutubia...

Habari za SiasaTangulizi

Wizara Katiba na Sheria yaliomba Bunge Sh. 441.2 bilioni

Spread the love  WIZARA ya Katiba na Sheria imeliomba Bunge liidhinishe bajeti...

error: Content is protected !!