Saturday , 2 December 2023
Home Gazeti Tangulizi Serikali yatangaza bomoa bomoa Dar-Arusha
Tangulizi

Serikali yatangaza bomoa bomoa Dar-Arusha

Mkurugenzi wa  TRL,  Masanja  Kadogosa
Spread the love

KAMPUNI ya Reli (TRL), imetangaza kubomoa nyumba zote zilizojengwa kando kando mwa reli inayotoka Dar es salaam, Moshi  hadi jijini Arusha, anaandika Angela Willium.

Kadhalika, TRL imetangaza kuanza kuifanyia ukarabati mkubwa reli hiyo ili ianze kutumika kusafirishisha mizigo kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam , Mkurugenzi wa  TRL,  Majanja  Kadogosa katika ziara  ya   Naibu Waziri wa Ujenzi  ,Uchukuzi na Mawasiliano,  Atashasta Nditiye amesema  baadhi ya nyumba zilizopo kwenye eneo la reli wameshaziwekea alama ya X.

Amesema alama ya X imeweka katika mikoa ya Morogoro na Dodoma ambapo inajengwa reli kubwa ambayo itapitisha Treni ya kutumia umeme.

“Tunawaomba wananchi waliovamia maeneo ya reli kuondoka mapema kabla ya kuanza zoezi la bomoa bomoa  nyumba zao tumeshaziweka alama ya X”.

Kadogosa amesema wamekuwa na changamoto ya ubovu wa reli pamoja na upungufu wa wafanyakazi na kuomba waboreshewe maslai ya watumishi.

Kuhusu ujenzi wa reli ya mikoa ya Kaskazini, alisema wameshaanza na kwamba hivi sasa wamefika Mombo na itachukua miezi  7 hadi 8  kukamilika.

Kwa upande wake, Nditiye amesema kutokana na changamoto iliyopo ya kuwaondoa wananchi waliovamia eneo la reli aliwaomba kupisha na kwamba ambao wataingiliwa na reli watalipwa fidia.

Ukarababti wa reli ya Moshi hadi Arusha  utakamilika ifikapo mwaka 2019 na lengo la ujenzi huo ni kukuza uchumi wa Tanzania na kutoa huduma kwa wananchi kwani gari moshi itabeba mizigo na nyingine  itachukua abiria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Mwalimu jela miaka mitatu kwa rushwa

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mfawidhi, wilaya ya Igunga, mkoani Tabora imemhukumu...

Habari za SiasaTangulizi

⁩ Samia aridhia Chongolo kujiuluzu

Spread the loveMwenyekiti wa CCM, Rais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano ameridhia...

Habari MchanganyikoTangulizi

13 wafariki dunia ajali ya basi likigonga treni Singida

Spread the loveJUMLA ya watu 13 wakiwamo wanawake sita na wanaume saba...

Habari MchanganyikoTangulizi

33 wanusurika ajali ya ndege Mikumi

Spread the loveJUMLA ya abiria 30, marubani wawili na mhudumu mmoja wamenusurika...

error: Content is protected !!