Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Jinamizi lamkalia Diallo uenyekiti CCM  Mwanza
Habari MchanganyikoTangulizi

Jinamizi lamkalia Diallo uenyekiti CCM  Mwanza

Anthony Diallo, Mmiliki wa Sahara Media ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza,
Spread the love

JINAMIZI la kisiasa limezidi kumkalia kooni mwenyekiti wa sasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoa wa Mwanza, Antony Diallo baada ya kuibuka tuhuma dhidi yake kwamba  ameanza kampeni za kumchafua mgombea mwenzake,  Meck Sadik, anaandika Moses Mseti.

Sadik alikuwa  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro katika utawala wa awamu ya tano ya Rais John Magufuli, lakini aliachia nafasi hiyo kwa madai kwamba ameamua kupumzika.

Diallo anadaiwa kumchafua Sadik kwa kusema kwamba ni pandikizi la aliyekuwa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.

Mikosi ya kisiasa ilianza kumuandama Diallo tangu mwaka 2010 aliposhindwa nafasi ya ubunge na kiti chake kuchukuliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Taarifa zinaeleza kwamba, tangu Diallo ashindwe kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 na aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Highness Kiwia (Chadema) ameendelea kuporomoka na ushawishi wake ndani na nje ya mkoa umeshuka.

Hata hivyo tuhuma hizo hazikuthibitishwa kutokana na Diallo kutopatikana kwenye simu zake ili kuzungumzia tuhuma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

error: Content is protected !!