Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wauzaji kuku Singida wapaza sauti
Habari Mchanganyiko

Wauzaji kuku Singida wapaza sauti

Kuku wa kienyeji
Spread the love

WAFANYABIASHARA wa soko la kuku mkoani Singida wameiomba Serikali kuangalia na kuboresha upatikanaji wa masoko ya uhakika hapa nchini, anaandika Christina Haule.

Ombi hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa soko hilo, Shabani Mahiki wakati akizungumza na viongozi na waandishi kutoka klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (MoroPC) na Singida SingPress walipotembelea kwenye soko hilo kuona faida na manufaa wanayopata wafanyabaishara hao.

Mahiki alisema wafanyabiashara wanaosafirisha kuku kwenye matenga kwenda mkoa mbalimbali hasa jijini Dar es salaam wanunuzi wamekuwa siyo waaminifu.

“Utakuta mmetuma mzigo labda tenga zenye thamani ya shilingi milioni moja halafu mtu anapokea mzigo na baada ya wiki kadhaa anakutumia laki tano badala ta kukutumia zote,” amesema Mahiki.

Muuzaji wa kuku katika soko hilo, Jumanne Mkotya aliiomba Serikali kuondoa au kufuta ushuru kwa biashara ya kuku.
Mkotya amesema, usafirishaji wa kuku mikoani husababisha baadhi ya kuku kufa njiani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!