Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Wauzaji kuku Singida wapaza sauti
Habari Mchanganyiko

Wauzaji kuku Singida wapaza sauti

Kuku wa kienyeji
Spread the love

WAFANYABIASHARA wa soko la kuku mkoani Singida wameiomba Serikali kuangalia na kuboresha upatikanaji wa masoko ya uhakika hapa nchini, anaandika Christina Haule.

Ombi hilo lilitolewa na Mwenyekiti wa soko hilo, Shabani Mahiki wakati akizungumza na viongozi na waandishi kutoka klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Morogoro (MoroPC) na Singida SingPress walipotembelea kwenye soko hilo kuona faida na manufaa wanayopata wafanyabaishara hao.

Mahiki alisema wafanyabiashara wanaosafirisha kuku kwenye matenga kwenda mkoa mbalimbali hasa jijini Dar es salaam wanunuzi wamekuwa siyo waaminifu.

“Utakuta mmetuma mzigo labda tenga zenye thamani ya shilingi milioni moja halafu mtu anapokea mzigo na baada ya wiki kadhaa anakutumia laki tano badala ta kukutumia zote,” amesema Mahiki.

Muuzaji wa kuku katika soko hilo, Jumanne Mkotya aliiomba Serikali kuondoa au kufuta ushuru kwa biashara ya kuku.
Mkotya amesema, usafirishaji wa kuku mikoani husababisha baadhi ya kuku kufa njiani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!