Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Sheikh Ponda atii sheria bila shuruti, ajisalimisha Polisi
Habari za SiasaTangulizi

Sheikh Ponda atii sheria bila shuruti, ajisalimisha Polisi

Sheikh Ponda, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Taasisi za Kiislam Tanzania
Spread the love

SHEIKH Issa Ponda, Katibu Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania amethibitisha kuwa anaheshimu mamlaka na sheria kutokana kutii wito wa Jeshi la Polisi, anaandika Faki Sosi.

Sheikh Ponda amewasili Kituo kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam majira ya saa nne asubuhi.

Wito huo ulitolewa Jana na Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari ambapo alimpa siku tatu kujisalimisha kituoni hapo.

Juzi Jeshi la Polisi lilivamia mkutano uliofanywa na Sheikh Ponda na waandishi wa habari kwenye Hotel ya Iris jijini Dar es Salaam kwa lengo la kumtia mbaroni.

Hata hivyo Polisi walimkosa Sheikh Ponda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

error: Content is protected !!