Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mchengerwa alia tatizo la umeme Rufiji
Habari Mchanganyiko

Mchengerwa alia tatizo la umeme Rufiji

Fundi umeme wa Tanesco akiunganisha umeme wa REA katika moja ya nyumba zilizopo kijijini
Spread the love

MBUNGE wa Rufiji Mohammed Mchengerwa(CCM) amehoji ni lini serikali itawaunganisha wananchi wa Rufiji,Kibiti na Kilwa kwenye grid ya taifa, anaandika Dany Tibason.

Akiuliza swali jana bungeni, kwa niaba ya Mchengerwa,Mbunge wa Kilolo,Venance Mwamoto(CCM) alidai ni takribani miaka miwili sasa serikali imeshindwa kuwahakikishia wananchi wa jimbo la Rufiji kuwa na umeme wa uhakika.

“Je ni lini serikali itawaunganisha wananchi wa Rufiji, Kibiti na Kilwa kwenye Grid ya Taifa,’? aliuliza

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Dk Medard Kalemani, amesema Wilaya za Kilwa, Rufiji na Kibiti, zitaunganishwa katika gridi ya taifa kupitia utekelezaji wa mradi wa ujenzi kutoka Somanga,Fungu(Lindi) hadi Kinyerezi Dar es salaam.

“Mradi huu utaunganisha na kusafirisha umeme utakaozalishwa katika Kituo cha Somanga, Fungu kwenye uwezo wa kuzalisha MW 240,”alisema

Amesema kazi inayofanywa kwa sasa ni pamoja na kukamilisha malipo ya fidia kwa wananchi watakaopitisha mradi na kwamba kazi ya ujenzi huo inatarajiwa kuanza Julai 2018 na kukamilika Desemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!