Wednesday , 6 December 2023
Home Habari Mchanganyiko TRA kuwashukia waendesha Bahati Nasibu
Habari Mchanganyiko

TRA kuwashukia waendesha Bahati Nasibu

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi, wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Richard Kayombo
Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imeanza kutekeleza jukumu la kukusanya kodi kwenye michezo ya kubahatisha jukumu ambalo ilikabidhiwa kuanzia mwezi Julai mwaka huu anaandika Irene Emmanuel.

Akiongea na waandishi wa Habari leo jijini Dar es salaam, Richard Kayombo, Mkurugenzi Huduma na Elimu kwa Mlipakodi amesema kwamba kutokana na nmabadiliko hayo TRA itakusanya kodi katika michezo yote ya kubahatisha ikiwemo casino, sports betting, slot machines, lottery na kupitia ujumbe mfupi wa kwenye simu (sms).

“Mshindi katika bahati nasibu atakatwa asilimia 18 ya kiasi alichoshinda na kuwasilishwa TRA na mchezaji bahati nasibu huyo na kwa upande wa wachezeshaji kuwasilisha asilimia ya mapato, casino 15%, sports betting 6%, SMS na lottery 30%, National lottery 10% na vslot machines ni 32,000/- kila mwezi.” Kayombo Aliongeza.

TRA ikishirikiana na bodi ya michezo ya kubahatisha imetoa na inaendelea kutoa mafunzo kwa wananchi na waendeshaji wa michezo hiyo na piainatoa wito kwa wahusika wote kutoa ushirikiano ili kufasnikisha ukusanyaji wa mapato kwa ufanisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

error: Content is protected !!