Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Viziwi wapewa elimu ya kilimo
Habari Mchanganyiko

Viziwi wapewa elimu ya kilimo

Mashine ya kuvutia maji kwaajili ya umwagiliaji
Spread the love

CHAMA cha Maendeleo ya Kilimo kwa Viziwi Tanzania (CHAMAKIVITA) kimejipanga kutoa elimu kwa viziwi ili kuwawezesha kulima kilimo cha kisasa, anaandika Dany Tibason.

Kelvin Nyema ambaye ni kiongozi mtendaji wa chama hicho alisema kuwa chama hicho kimejipanga kutoa elimu kwa viziwi ambao ni wakulima kwa lengo la kuwaodolea changamoto wanazokumbana nazo.

Nyema amesema licha ya viziwi kujihusisha na kilimo, lakini wamejikuta wakilima bila kuwa na tija kutokana na kutokuwa na elimu ya kuhusu kilimo na kutokujua msimu halisi.

Amesema kutokana na changamoto mbalimbali za kimawasiliano viziwi wengi ambao wamekuwa hawajui namna bora ya kulima kilimo cha kisasa ikiwa ni pamoja na kutofahamu majira halisi ya kilimo.

“Tumelazimika kuanzisha chama cha maendeleo ya kilimo kwa viziwi Tanzania kwa lengo la kuwakwamua viziwi ambao wanajihusisha na kilimo,wakulima wengi ambao ni viziwi wanalima lakini kilimo chao bado ni duni.

“Kutokana na changamoto hizo kwa sasa tutatoa elimu kwa wakulima ambao ni viziwi kwa lengo la kuwafanya wakulima hao walime kilimo cha kisasa na kutumia pembejeo ambazo zinaendana na msimu wa kilimo.

“Kama viziwi watapatiwa elimu bora ya kilimo wataweza kulima kilimo bora na kuwaondolea dhana kwamba kundi hilo ni wategemezi, tunatazamia washiriki 300 watapatiwa elimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

error: Content is protected !!