Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema atinga uraiani
Habari za Siasa

Mbunge Chadema atinga uraiani

Wabunge Ester Bulaya na Halima Mdee
Spread the love

HATIMAYE mbunge wa Bunda (Chadema), Ester Bulaya amepata dhamana baada ya kushikiliwa na Polisi kanda maalum ya Tarime na Rorya kwa amri ya Mkuu wa wilaya ya hiyo Glorious Luoga, anaandika Mwandishi Wetu.

Kabla ya kupata dhamana leo hii, wanachama wa Chadema kutoka maeneo mbalimbali mkoani Mara ikiwamo jimboni kwake, walifurika kituo cha polisi.

Kutokana na wingi wa wananchi hao wakiongozwa na Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche, polisi wameonekana kuweka ulinzi mkali.

mwishoni mwa wiki, Bulaya alikamatwa na jeshi la Polisi akiwa katika Hotel ya Kifa Best Point Wilayani Tarime akidaiwa kujiandaa kutaka kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.

Kamanda wa polisi Tarime/Rorya Kamishina Msaidizi Mwandamizi Henry Mwaibambe alisema Bulaya hakutakiwa kushiriki katika mkutano wa Ester Matiko (Chadema), ambaye ni mbunge wa Tarime mjini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!