Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa MCT wamtia hatiani Makonda
Habari za SiasaTangulizi

MCT wamtia hatiani Makonda

Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga. Picha ndogo, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limezidi kumkaanga Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Mkaonda baada ya kubaini kwamba alihusika moja kwa moja kuvamia Clouds Media Group, anaandika Faki Sosi.

Mwezi Machi mwaka huu, Tume maalum iliyoundwa na aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ilitoa ripoti kama ya MCT.

Katika ripoti yake, MCT imebaini Makonda alihusika kufanya uvamizi huo na wamejiridhisha pasipo kuacha shaka na kwamba hawajamuonea.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema kuwa ripoti hiyo hajamuonea Makonda.

“Hatujafanya utafiti huu kwa sababu tunamahaba maalum na Clouds au tunamahaba na mkuu wa mkoa na kwamba huu sio utafiti wa kwanza tulianza kwa marehemu Daudi Mwangosi alipouwa,” amesema

”Sisi kwetu haijarishi watu wameelewana au hawajaelewana sisi kwetu tunaangalia uvamizi huu jinsi ilivyoathiri vyombo vya habari”, amesema Mukajanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!