JESHI la Polisi Kanda maalum ya jijini Dar es Salaam limeahidi kupambana na wapiga debe katika vituo mbalimbali vya mabasi na kuwakamata, anaandika Irene Emmanuel.
Hayo yamesemwaka leo na Kamanda wa Polisi kanda hiyo, Lucas Mkondya na kewamba kazi ya kuwasaka wapiga debe imeanza katika vituo vya mabasi.
Akizungumza na MwanaHALISI online, Mkondya amesema kuna mbinu nyingi ambazo watazitumia kupambana na wapiga debe hadi kuhakikisha wameondoka wote.
Amesema hawezi kusema mbiunu watakazotumia katika kufanikisha kazi hiyo, lakini akaahidi kwamba haitakuwa na kikomo.
‘Tukiwatoa huku wakajidanganya kukimbilia mtaani watakutana na sisi tena, kwa hiyo wao wafanye kazi zilizo halali na siyo za uhalifu kwani tutapambana nao.,” Mkondya ameeleza.
Amesema tayari wameishaanza kazi katika baadhi ya vituo vya mabasi ikiwemo Mwenge jijini Dar es Salaam.
Hii siyo mara ya kwanza jeshi la polisi kupiga marufuku uwepo wa wapiga debe katika vituo vya mabasi bila mafanikio.
Leave a comment