Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa MCT wamtia hatiani Makonda
Habari za SiasaTangulizi

MCT wamtia hatiani Makonda

Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga. Picha ndogo, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limezidi kumkaanga Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Mkaonda baada ya kubaini kwamba alihusika moja kwa moja kuvamia Clouds Media Group, anaandika Faki Sosi.

Mwezi Machi mwaka huu, Tume maalum iliyoundwa na aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ilitoa ripoti kama ya MCT.

Katika ripoti yake, MCT imebaini Makonda alihusika kufanya uvamizi huo na wamejiridhisha pasipo kuacha shaka na kwamba hawajamuonea.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema kuwa ripoti hiyo hajamuonea Makonda.

“Hatujafanya utafiti huu kwa sababu tunamahaba maalum na Clouds au tunamahaba na mkuu wa mkoa na kwamba huu sio utafiti wa kwanza tulianza kwa marehemu Daudi Mwangosi alipouwa,” amesema

”Sisi kwetu haijarishi watu wameelewana au hawajaelewana sisi kwetu tunaangalia uvamizi huu jinsi ilivyoathiri vyombo vya habari”, amesema Mukajanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!