Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa MCT wamtia hatiani Makonda
Habari za SiasaTangulizi

MCT wamtia hatiani Makonda

Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga. Picha ndogo, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limezidi kumkaanga Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Mkaonda baada ya kubaini kwamba alihusika moja kwa moja kuvamia Clouds Media Group, anaandika Faki Sosi.

Mwezi Machi mwaka huu, Tume maalum iliyoundwa na aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ilitoa ripoti kama ya MCT.

Katika ripoti yake, MCT imebaini Makonda alihusika kufanya uvamizi huo na wamejiridhisha pasipo kuacha shaka na kwamba hawajamuonea.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema kuwa ripoti hiyo hajamuonea Makonda.

“Hatujafanya utafiti huu kwa sababu tunamahaba maalum na Clouds au tunamahaba na mkuu wa mkoa na kwamba huu sio utafiti wa kwanza tulianza kwa marehemu Daudi Mwangosi alipouwa,” amesema

”Sisi kwetu haijarishi watu wameelewana au hawajaelewana sisi kwetu tunaangalia uvamizi huu jinsi ilivyoathiri vyombo vya habari”, amesema Mukajanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!