Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Wakenya wabaini  akili za kuambiwa changanya na zako
Makala & Uchambuzi

Wakenya wabaini  akili za kuambiwa changanya na zako

Raila Odinga, aliyekuwa mgombea wa Muungano wa NASA
Spread the love

WAFUASI wa aliyekuwa mgombea urais nchini Kenya, Raila Odinga wamepuuza kauli yake iliyowataka leo kutoenda kazini, anaandika Victoria Chance.

Odinga aliwataka wafuasi wake kususa kwenda kazini kama ishahara ya kupinga alichodai ni kuibiwa kura katika uchaguzi mkuu uliofanyika wiki iliyopita.

Katika uchaguzi huo, aliyekuwa mgombea wa kiti hicho kupitia muungano wa Jubilee, Uhuru Kenyatta aliibuka mshindi.

Tofauti na hali ilivyokuwa wiki iliyopita, leo maeneo mbalimbali jijini Nairobi ikiwemo mitaa ya Mathare, Kibera wananchi wameanza kufanya shughuliu zao.

Baadhi ya wakazi wa maeneo hayo wamesema  wanahitaji kufanya kazi ili wapate chakula na mahitaji mengine ya msingi huku baadhi yao wakitii kauli ya Odinga.

Aidha, uongozi wa NASA umedai kuwa mitambo ya tume ya uchaguzi haikutenda haki katika kumfanya Kenyatta awe mshindi hivyo wataenda kortini kupinga matokeo hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMakala & Uchambuzi

Kanda ya Ziwa yaonyesha NMB inavyosaidia afya ya mama na mtoto

Spread the loveMafanikio inayozidi kupata Tanzania katika kupunguza vifo vya mama na...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

‘Mwanapekee’ wa Rais Samia: Atabadili nini Arusha?

Spread the loveMAPEMA wiki hii, baadhi ya viongozi walioapishwa na Rais Samia...

Habari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kipunguni waihoji serikali, ziko wapi fedha za fidia?

Spread the loveWATU wanaodai kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ni sikivu,...

Habari za SiasaMakala & UchambuziTangulizi

Askofu Bagonza: Tusichonganishwe; tusichokozane na tusikufuru

Spread the loveJOTO la chaguzi linapanda kila siku hapa nchini. Upo umuhimu...

error: Content is protected !!