Sunday , 5 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Meena awaomba radhi wanahabari
Habari MchanganyikoTangulizi

Meena awaomba radhi wanahabari

Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam (katikati) akizungumza na Theophil Makunga, Mwennyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania na Naville Meena, Katibu wa Jukwaa hilo
Spread the love

NEVILE Meena, Katibu Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), amewaomba radhi waandishi wa habari na Wahariri, anaandika Hellen Sisya.

Msamaha huo unafuatia Meena kutoa kauli kwamba kuanzia leo, wamemfungulia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye wanahabari walisusa kuandika habari zake.

Kauli hiyo ya kutaka Makonda afunguliwe iliyoonyesha kuwachukiza waandishi wa habari.
Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Meena ameandika ujumbe maalum wa kuomba radhi wanahabari.

Ametumia maneno ya kiingereza “We have messed up. My apologies to all journalists and media professionals” ameandika Meena.

Mapema leo hii Jukwaa hilo la wahariri liliitisha mkutano na wanahabari na kumfungulia kifungo RC Makonda, kifungo ambacho walimfungia kuandika na kuripoti taarifa zake.

Makonda alifungiwa baada ya kuvamia kituo cha TV cha Clouds cha jijini Dar es Salaam na kutaka kulazimisha habari ya uongo kutangazwa dhidi ya  Mchungaji, Josephat Gwajima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!