Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Meena awaomba radhi wanahabari
Habari MchanganyikoTangulizi

Meena awaomba radhi wanahabari

Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam (katikati) akizungumza na Theophil Makunga, Mwennyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania na Naville Meena, Katibu wa Jukwaa hilo
Spread the love

NEVILE Meena, Katibu Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), amewaomba radhi waandishi wa habari na Wahariri, anaandika Hellen Sisya.

Msamaha huo unafuatia Meena kutoa kauli kwamba kuanzia leo, wamemfungulia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye wanahabari walisusa kuandika habari zake.

Kauli hiyo ya kutaka Makonda afunguliwe iliyoonyesha kuwachukiza waandishi wa habari.
Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Meena ameandika ujumbe maalum wa kuomba radhi wanahabari.

Ametumia maneno ya kiingereza “We have messed up. My apologies to all journalists and media professionals” ameandika Meena.

Mapema leo hii Jukwaa hilo la wahariri liliitisha mkutano na wanahabari na kumfungulia kifungo RC Makonda, kifungo ambacho walimfungia kuandika na kuripoti taarifa zake.

Makonda alifungiwa baada ya kuvamia kituo cha TV cha Clouds cha jijini Dar es Salaam na kutaka kulazimisha habari ya uongo kutangazwa dhidi ya  Mchungaji, Josephat Gwajima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!