Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Meena awaomba radhi wanahabari
Habari MchanganyikoTangulizi

Meena awaomba radhi wanahabari

Paul Makonda, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam (katikati) akizungumza na Theophil Makunga, Mwennyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania na Naville Meena, Katibu wa Jukwaa hilo
Spread the love

NEVILE Meena, Katibu Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), amewaomba radhi waandishi wa habari na Wahariri, anaandika Hellen Sisya.

Msamaha huo unafuatia Meena kutoa kauli kwamba kuanzia leo, wamemfungulia Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye wanahabari walisusa kuandika habari zake.

Kauli hiyo ya kutaka Makonda afunguliwe iliyoonyesha kuwachukiza waandishi wa habari.
Katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, Meena ameandika ujumbe maalum wa kuomba radhi wanahabari.

Ametumia maneno ya kiingereza “We have messed up. My apologies to all journalists and media professionals” ameandika Meena.

Mapema leo hii Jukwaa hilo la wahariri liliitisha mkutano na wanahabari na kumfungulia kifungo RC Makonda, kifungo ambacho walimfungia kuandika na kuripoti taarifa zake.

Makonda alifungiwa baada ya kuvamia kituo cha TV cha Clouds cha jijini Dar es Salaam na kutaka kulazimisha habari ya uongo kutangazwa dhidi ya  Mchungaji, Josephat Gwajima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

BiasharaTangulizi

TLS wajitosa sakata la ukodishaji wa bandari

Spread the love  CHAMA cha wanasheria Tanzania (TLS), kimejitosa katika sakata la...

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

error: Content is protected !!