Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba
Habari za SiasaTangulizi

Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge amebariki kuvuliwa uanachama kwa wabunge nane wa Chama cha Wananchi (CUF) na anayedai kuwa Mwenyekiti halali wa chama hicho, Prof. Ibrahimu Lipumba, anaandika Erasto Masalu.

Spika Ndugai amekubali barua aliyoandikiwa na Prof. Lipumba na Kaimu Katibu wake, Magdalena Sakaya ya kuwavua uanachama wabunge hao.

Kutokana na Spika Ndugai kukubali barua hiyo, wabunge Severina Silvanus Mwijage, Saumu Sakala, Salma Mwassa, Riziki Ngwali, Raisa Abdallah Mussa, Miza Bakari Haji, Hadija Ally Al-Qassmy na Halima Ali Mohamed wamekosa sifa ya kuwa wabunge.

Hatua hiyo inamaanisha kuwa Spika Ndugai anamtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF kama ilivyokuwa kwa msajiri wa vyama.

CUF wamekuwa na mgogoro ndani ya chama chao na tayari wana kesi mahakamani ya kutambua uongozi halali kati ya unaomtambua Prof. Lipumba na ule unaomuunga mkono Katibu wa chama hicho, Seif Sharrif Hamad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!