Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba
Habari za SiasaTangulizi

Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge amebariki kuvuliwa uanachama kwa wabunge nane wa Chama cha Wananchi (CUF) na anayedai kuwa Mwenyekiti halali wa chama hicho, Prof. Ibrahimu Lipumba, anaandika Erasto Masalu.

Spika Ndugai amekubali barua aliyoandikiwa na Prof. Lipumba na Kaimu Katibu wake, Magdalena Sakaya ya kuwavua uanachama wabunge hao.

Kutokana na Spika Ndugai kukubali barua hiyo, wabunge Severina Silvanus Mwijage, Saumu Sakala, Salma Mwassa, Riziki Ngwali, Raisa Abdallah Mussa, Miza Bakari Haji, Hadija Ally Al-Qassmy na Halima Ali Mohamed wamekosa sifa ya kuwa wabunge.

Hatua hiyo inamaanisha kuwa Spika Ndugai anamtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF kama ilivyokuwa kwa msajiri wa vyama.

CUF wamekuwa na mgogoro ndani ya chama chao na tayari wana kesi mahakamani ya kutambua uongozi halali kati ya unaomtambua Prof. Lipumba na ule unaomuunga mkono Katibu wa chama hicho, Seif Sharrif Hamad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!