Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba
Habari za SiasaTangulizi

Ndugai abariki timua timua ya Prof. Lipumba

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge amebariki kuvuliwa uanachama kwa wabunge nane wa Chama cha Wananchi (CUF) na anayedai kuwa Mwenyekiti halali wa chama hicho, Prof. Ibrahimu Lipumba, anaandika Erasto Masalu.

Spika Ndugai amekubali barua aliyoandikiwa na Prof. Lipumba na Kaimu Katibu wake, Magdalena Sakaya ya kuwavua uanachama wabunge hao.

Kutokana na Spika Ndugai kukubali barua hiyo, wabunge Severina Silvanus Mwijage, Saumu Sakala, Salma Mwassa, Riziki Ngwali, Raisa Abdallah Mussa, Miza Bakari Haji, Hadija Ally Al-Qassmy na Halima Ali Mohamed wamekosa sifa ya kuwa wabunge.

Hatua hiyo inamaanisha kuwa Spika Ndugai anamtambua Prof. Lipumba kama Mwenyekiti halali wa CUF kama ilivyokuwa kwa msajiri wa vyama.

CUF wamekuwa na mgogoro ndani ya chama chao na tayari wana kesi mahakamani ya kutambua uongozi halali kati ya unaomtambua Prof. Lipumba na ule unaomuunga mkono Katibu wa chama hicho, Seif Sharrif Hamad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!