TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, hatimaye amepata dhamana baada ya ombi la mawakili wa serikali la kuomba mahakam imnyime dhamana kutupiliwa mbali, anaandika Hellen Sisya.
Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri amesema, baada ya kupitia hoja za serikali na majibu ya mawakili wa utetezi, haoni mantiki ya kuzuia dhamana kwa Lissu.
Hivyo, Hakimu Mashauri amemtaka Lissu kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika ambapo kila mmoja atasaini bondi ya Sh. 10 milioni.
Lissu ametimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana, lakini anatakiwa kupewa kibali cha mahakama kila anapotaka kutoka nje ya Dar es Salaam.
Kesi itasikilizwa Agosti 24, 2017 na upande wa serikali imesema upepelezi wa kesi hiyo umekamilika.
Baada ya kuachiwa Lissu na mawakili wake wamezuiwa kuzungumza nje ya mahakama.
Leave a comment