Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani Kongwa wamtega Rais Magufuli
Habari za Siasa

Madiwani Kongwa wamtega Rais Magufuli

Mfano wa reli itakayotumika na treni ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro
Spread the love

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, limemuomba Rais John Magufuli kujenga reli ya treni ya abiria ya mwendo kasi kuanzia Dodoma mjini hadi mji mdogo wa Kibaigwa mkoani humo, anaandika Dany Tibason.

Madiwani hao wamesema ni bausara reli hiyo kufika Kibaigwa ambako kuna soko kubwa la mahindi badala ya kuishia Bwigiri wilayani Chamwino ili kurahisisha wafanyabiashara wa mahindi kusafirisha mizigo yao kwa urahisi.

Wakizungumza katika kikao cha Baraza hilo Madiwani hao walisema ujenzi wa reli hiyo hadi Kibaigwa utakuwa ni faraja kwa wananchi hususani wafanyabiashara wanaopeleka mazao katika soko la Kibaigwa.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, White Zuberi amesema soko la Kibaigwa lina wafanyabiashara wengi kutoka maeneo mbalimbali katika mkoa wa Dodoma na ambao wamekuwa wakipata shida kusafirisha mazao yao kuelekea katika soko hilo.

“Mheshimiwa Rais Magufuli ameahidi kujenga reli ya treni ya abiria kutoka Dodoma mjini hadi Bwigiri, lakini na sisi wanakongwa tunamuomba rais kujenga reli hiyo hadi Kibaigwa ambako kuna soko kubwa la mahindi ili kusogeza karibu huduma ya usafiri kwa wafanyabiashara wanaofika sokoni hapo,” amesema Zuberi

Pia Zuberi amesema reli hiyo itakapofika katika mji mdogo wa Kibaigwa itarahisisha usafiri kwa wananchi wa kawaida kwa kuwa hivi sasa kuna shida ya usafiri kati ya hapo na Dodoma mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kufumua mitaala ya vyuo vikuu, ufundi stadi

Spread the loveSERIKALI inakusudia kufanya mapitio katika mitaala na programu za vyuo...

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

error: Content is protected !!