Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tundu Lissu kumkuta ya Lema?
Habari za SiasaTangulizi

Tundu Lissu kumkuta ya Lema?

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema (katikati mwenye fulana nyekundu) akiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri kusikiliza shauri lake
Spread the love

TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, amenyimwa dhamana baada ya kufikishwa katika Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam na kusomewa mashtaka ya kutoa lugha ya uchochezi ambayo imesababisha chuki kwa jamii, anaandika Hellen Sisya.

Akisomewa mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri leo Jumatatu, Julai 24, mahakama imeelezwa kuwa Lissu alitoa lugha ya uchochezi dhidi ya serikali Julai 17 akiwa maeneo ya Ufipa, Kinondoni.

Imedaiwa kuwa maneno hayo yalikuwa na lengo la kuleta chuki kwenye jamii kwa kuwa Lissu alisema Rais John Magufuli anateua viongozi kwa kuangalia familia, kabila na ukanda.
Lissu alikana shtaka hilo huku akisema, kusema ukweli hakijawahi kuwa kosa la jinai kwa hiyo siyo kweli.

Lissu amenyimwa dhamana baada ya mawakili wa serikali kuwasilisha hoja za kuiomba mahakama hiyo, imnyime.

Hata hivyo, upande wa mawakili wa mshtakiwa kujaribu kumnusuru asiende mahabusu ziligonga mwamba.

Baada ya Lissu kupelekwa Lumande, mahakama hiyo itatoa uamuzi kuhusu dhamana Julai 27 mwaka huu ambapo Hakimu atatoa maamuzi ya hoja za mawakili wa serikali.

Wiki iliyopita Lissu alikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa anataka kwenda nchini Rwanda kuhudhuria mkutano wa Wanasheria Afrika Mashariki.

Godbless Lema, Mbunge wa Arusha Mjini aliwahi kukaa rumande kwa zaidi miezi minne bila dhamana baada ya kuibuka na mvutano wa mawakili wa serikali na wanaomtetea, aliposhtakiwa kwa kosa la kuoteshwa kuwa Rais John Magufuli atakufa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!