Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu wanaorubuni wanafunzi kukiona
Elimu

Walimu wanaorubuni wanafunzi kukiona

Mwanafunzi mwenye Mimba
Spread the love

SERIKALI Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma  imeahidi kuwachukulia hatua za kisheria walimu wote ambao watatajwa kujihusisha kimapenzi na watoto wa kike wanaosoma katika shule zote, anaandika Mwandishi Wetu.

Aidha, amewataka walimu ambao wanajiona kuwa na mahitaji ya kufanya mapenzi na hawajui maeneo ya kupata wanawake kupeleka maombi ofisini kwake na yeye atafanya taratibu za kuwatafutia wanawake ambao wamekuwa wakijiuza.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera wakati akizungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya Sekondari Mtutura iliyopo katika Kata ya Namiungo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi na uhamasishaji wa maendeleo.

Katika taarifa hiyo Dc, Homera aliitaja Shule ya Kutwa ya Frank Weston mini hapa kuwa imekuwa ni miongoni mwa shule zinazotajwa kuwa ni kituo cha Mapenzi kati yao na wanafunzi.

Amesema walimu wanne wa shule hiyo ingawa hakuwataja majina yao wamekwisha simamisha kazi baada ya kutuhumiwa kuwa na mahusiano na wanafunzi shuleni hapo.

Hata hivyo, Homera aliwataka watoto wa kike kuzingatia masomo na kwamba endapo watashindwa kusoma wajue kwamba wameumia kwani watashindwa kuzifikia ndoto zao kielimu.

Amesema ndoto zao hazitazimia endapo watabainika kupata ujauzito kwa kuwa serikali ina mpango wa kuwapima kipimo watoto wote wa kike wiki mbili au moja kabla ya kipindi cha kufanya mitihani ya kidato cha Pili na cha Nne kila mwaka na kuwaondoa watakaobainika kuwa na mimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!