Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Walimu wanaorubuni wanafunzi kukiona
Elimu

Walimu wanaorubuni wanafunzi kukiona

Mwanafunzi mwenye Mimba
Spread the love

SERIKALI Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma  imeahidi kuwachukulia hatua za kisheria walimu wote ambao watatajwa kujihusisha kimapenzi na watoto wa kike wanaosoma katika shule zote, anaandika Mwandishi Wetu.

Aidha, amewataka walimu ambao wanajiona kuwa na mahitaji ya kufanya mapenzi na hawajui maeneo ya kupata wanawake kupeleka maombi ofisini kwake na yeye atafanya taratibu za kuwatafutia wanawake ambao wamekuwa wakijiuza.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Juma Homera wakati akizungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya Sekondari Mtutura iliyopo katika Kata ya Namiungo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi na uhamasishaji wa maendeleo.

Katika taarifa hiyo Dc, Homera aliitaja Shule ya Kutwa ya Frank Weston mini hapa kuwa imekuwa ni miongoni mwa shule zinazotajwa kuwa ni kituo cha Mapenzi kati yao na wanafunzi.

Amesema walimu wanne wa shule hiyo ingawa hakuwataja majina yao wamekwisha simamisha kazi baada ya kutuhumiwa kuwa na mahusiano na wanafunzi shuleni hapo.

Hata hivyo, Homera aliwataka watoto wa kike kuzingatia masomo na kwamba endapo watashindwa kusoma wajue kwamba wameumia kwani watashindwa kuzifikia ndoto zao kielimu.

Amesema ndoto zao hazitazimia endapo watabainika kupata ujauzito kwa kuwa serikali ina mpango wa kuwapima kipimo watoto wote wa kike wiki mbili au moja kabla ya kipindi cha kufanya mitihani ya kidato cha Pili na cha Nne kila mwaka na kuwaondoa watakaobainika kuwa na mimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!