Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi walikoroga Ruvuma, wazuia vikao vya ndani vya Chadema
Habari za Siasa

Polisi walikoroga Ruvuma, wazuia vikao vya ndani vya Chadema

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limekizuia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kufanya mikutano ya ndani, anaandika Irene David.

Katazo hilo limekuja siku chache baada ya viongozi waandamizi wa chama waliokuwa mkoani humo akiwamo Katibu Mkuu, Vicent Mashinji kushikiliwa na vyombo vya usalama kwa madai kwamba wanatumia lugha za kashfa na matusi kwa viongozi wa umma.

Kwa mujibu wa barua ya Kamanda wa Polisi iliyotumwa kwa Mkuu wa Mkoa huo, IGP  na Ofisa Usalama wa Taifa, ni marufuku viongozi hao kufanya mikutano ya ndani.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gemini Mushy, amesema viongozi hao wa Chadema wanafanya shughuli zao kinyume cha sheria ya polisi sura 322 fungu 43(4).

Alisema sheria hiyo unawapa polisi mamlaka ya  kuchukua  hatua za  kuzuia shughuli kama hizo.

Kamanda huyo katika taarifa amesema viongozi hao wataruhusiwa pale  jeshi la polisi litakapojiridhisha kwamba wanafuata maelekezo yanayoendana na vikao vya ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!