Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko BAKWATA yampinga “Mtume wa uongo” Pwani
Habari Mchanganyiko

BAKWATA yampinga “Mtume wa uongo” Pwani

Msemaji Mkuu wa Mufti, Khamis Mataka
Spread the love

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limewataka waumini wake na watanzania wote nchini kumpuuza mtu mmoja aliyejitokeza huko mkoani Pwani, akidai kuwa yeye ni Nabii Ilyasa, anaandika Irene David.

Mwenyekiti wa Halmashauri BAKWATA taifa na Msemaji Mkuu wa Mufti, Khamis Mataka, amethibitisha kuwepo na upotoshwaji wa mafundisho ya Uislamu yatolewayo na Hamza Issa, “Mtume Ilyasa” wakati akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya baraza hilo jijini Dar es Salaam.

Issa anadai kuwa yeye ni Muislam amepewa ufunuo na kwamba roho ya ”Mtume Ilyasa” imemuingia na hivyo yeye ndiye “Nabii Ilyasa” mwenyewe.

Anatumia Qurani na mafunzo ya kiislamu jambo lililosababisha Baraza la Masheihk wa mkoa wa Pwani kutolifumbia macho na kuleta maazimio yao kwa Mufti Mkuu.

Kwa mujibu wa Imani yetu sisi Waislam, tunaamini kuwa hakuna Nabii aliyekuwepo na atakaye kuja kuwepo tena zaidi ya Nabii na Mtume Mohammad.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!