Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya wa jiji atoa siku 12 kwa wakwepa kodi
Habari za Siasa

Meya wa jiji atoa siku 12 kwa wakwepa kodi

Mwita Isaya, Meya wa Jiji la Dar es Salaam (aliyesimama) akizungumza na wafanyabishara wa stendi ya Ubungo
Spread the love

MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Issaya Mwita ametoa siku 12 kwa wafanyabiashara wasiolipa kodi katika Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kuhakikisha wanalipa vinginevyo atawachukulia hatua kali, anaandika, Jovina Patrick.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kushtukiza akiwa ameambatana na Kamati ya Uongozi na Fedha ya Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza na wafanyabiashara hao, Mwita amesema kuwa wasipolipa kodi hiyo ifikapo Agosti hatua kali juu dhidi yao zitachukuliwa kwani baadhi yao kuna wadaiwa sugu.

Anasema “Na itakapofika mwezi wa nane nitaagiza wasaidizi wangu na yeyote atakayekuwa hajalipa kodi hatua kali zichukuliwe juu yake”.

Meya amewaonya wafanyabiashara hao juu ya ukaidi wao kutolipa kodi na kusema kuongeza kuwa fedha wanazolipa ni kwa ajili ya manufaa yao wenyewe .

“Pesa hiyo mnayolipa ndiyo inayonunulia umeme, kulipia maji, usafi wa vyoo ni wajibu wenu kulipa kodi,” amesema Meya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!