Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafanyabiashara Ubungo wacharuka
Habari Mchanganyiko

Wafanyabiashara Ubungo wacharuka

Wafanyabiashara wa Kituo cha Mabasi cha Ubungo wakisubiri mkutano na Kamati ya Fedha ya Jiji la Dar es Salaam
Spread the love

MFANYABIASHARA ambaye pia ni Naibu katibu wa Wafanyabiashara kituo kikuu cha mabasi Ubungo jijini Dar es salaam, John Shayo ametangaza kuuburuza mahakamani uongozi wa kituo hicho kwa madi kuwa umetafuna fedha za wanazolipa kodi, anaandika, Irene Emmanuel.

Amesema anashangaa kuona anadaiwa deni kubwa la Sh. 800,000 wakati amelipa kodi zote.

“Haki yoyote inapatikana mahakamani, na mimi ninaweza kuwaambia hivi, huyu mtawala wa kituo ambaye ni meneja, mimi ndo nitakaye ‘mface’ zaidi kwa maana ameidanganya halmashauri, nitamfungulia mashtaka mahakamani,” amesema Shayo.

Akiongea na MwanaHALISI Online leo katika ziara ya kamati ya uongozi na fedha ya halmashauri ikiongozwa na Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, amesema kuwa mstahiki meya amedanganywa juu ya mikataba ya wapanganaji.

“Mstahiki Meya amedanganywa, nianze kuelezea hilo la mkataba, ule siyo mkataba, ni masharti magumu mno ambayo hawa wenzangu niliowabeba kama kiongozi wao hawawezi kuyatimiza” Shayo alieleza.

Aidha, Mstahiki Meya baada ya ziara hiyo, amewataka wafanyabiashara wote kituoni hapo kulipao madeni yao ya halmashauri hadi kufikia mwezi ujao na wasipotimiza hilo wataondolewa kwa nguvu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!