MFANYABIASHARA ambaye pia ni Naibu katibu wa Wafanyabiashara kituo kikuu cha mabasi Ubungo jijini Dar es salaam, John Shayo ametangaza kuuburuza mahakamani uongozi wa kituo hicho kwa madi kuwa umetafuna fedha za wanazolipa kodi, anaandika, Irene Emmanuel.
Amesema anashangaa kuona anadaiwa deni kubwa la Sh. 800,000 wakati amelipa kodi zote.
“Haki yoyote inapatikana mahakamani, na mimi ninaweza kuwaambia hivi, huyu mtawala wa kituo ambaye ni meneja, mimi ndo nitakaye ‘mface’ zaidi kwa maana ameidanganya halmashauri, nitamfungulia mashtaka mahakamani,” amesema Shayo.
Akiongea na MwanaHALISI Online leo katika ziara ya kamati ya uongozi na fedha ya halmashauri ikiongozwa na Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, amesema kuwa mstahiki meya amedanganywa juu ya mikataba ya wapanganaji.
“Mstahiki Meya amedanganywa, nianze kuelezea hilo la mkataba, ule siyo mkataba, ni masharti magumu mno ambayo hawa wenzangu niliowabeba kama kiongozi wao hawawezi kuyatimiza” Shayo alieleza.
Aidha, Mstahiki Meya baada ya ziara hiyo, amewataka wafanyabiashara wote kituoni hapo kulipao madeni yao ya halmashauri hadi kufikia mwezi ujao na wasipotimiza hilo wataondolewa kwa nguvu.
Leave a comment