Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Wafanyabiashara Ubungo wacharuka
Habari Mchanganyiko

Wafanyabiashara Ubungo wacharuka

Wafanyabiashara wa Kituo cha Mabasi cha Ubungo wakisubiri mkutano na Kamati ya Fedha ya Jiji la Dar es Salaam
Spread the love

MFANYABIASHARA ambaye pia ni Naibu katibu wa Wafanyabiashara kituo kikuu cha mabasi Ubungo jijini Dar es salaam, John Shayo ametangaza kuuburuza mahakamani uongozi wa kituo hicho kwa madi kuwa umetafuna fedha za wanazolipa kodi, anaandika, Irene Emmanuel.

Amesema anashangaa kuona anadaiwa deni kubwa la Sh. 800,000 wakati amelipa kodi zote.

“Haki yoyote inapatikana mahakamani, na mimi ninaweza kuwaambia hivi, huyu mtawala wa kituo ambaye ni meneja, mimi ndo nitakaye ‘mface’ zaidi kwa maana ameidanganya halmashauri, nitamfungulia mashtaka mahakamani,” amesema Shayo.

Akiongea na MwanaHALISI Online leo katika ziara ya kamati ya uongozi na fedha ya halmashauri ikiongozwa na Meya wa jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita, amesema kuwa mstahiki meya amedanganywa juu ya mikataba ya wapanganaji.

“Mstahiki Meya amedanganywa, nianze kuelezea hilo la mkataba, ule siyo mkataba, ni masharti magumu mno ambayo hawa wenzangu niliowabeba kama kiongozi wao hawawezi kuyatimiza” Shayo alieleza.

Aidha, Mstahiki Meya baada ya ziara hiyo, amewataka wafanyabiashara wote kituoni hapo kulipao madeni yao ya halmashauri hadi kufikia mwezi ujao na wasipotimiza hilo wataondolewa kwa nguvu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!