MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Issaya Mwita ametoa siku 12 kwa wafanyabiashara wasiolipa kodi katika Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kuhakikisha wanalipa vinginevyo atawachukulia hatua kali, anaandika, Jovina Patrick.
Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kushtukiza akiwa ameambatana na Kamati ya Uongozi na Fedha ya Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza na wafanyabiashara hao, Mwita amesema kuwa wasipolipa kodi hiyo ifikapo Agosti hatua kali juu dhidi yao zitachukuliwa kwani baadhi yao kuna wadaiwa sugu.
Anasema “Na itakapofika mwezi wa nane nitaagiza wasaidizi wangu na yeyote atakayekuwa hajalipa kodi hatua kali zichukuliwe juu yake”.
Meya amewaonya wafanyabiashara hao juu ya ukaidi wao kutolipa kodi na kusema kuongeza kuwa fedha wanazolipa ni kwa ajili ya manufaa yao wenyewe .
“Pesa hiyo mnayolipa ndiyo inayonunulia umeme, kulipia maji, usafi wa vyoo ni wajibu wenu kulipa kodi,” amesema Meya.
Leave a comment