Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya wa jiji atoa siku 12 kwa wakwepa kodi
Habari za Siasa

Meya wa jiji atoa siku 12 kwa wakwepa kodi

Mwita Isaya, Meya wa Jiji la Dar es Salaam (aliyesimama) akizungumza na wafanyabishara wa stendi ya Ubungo
Spread the love

MEYA wa Jiji la Dar es Salaam, Issaya Mwita ametoa siku 12 kwa wafanyabiashara wasiolipa kodi katika Kituo cha Mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo kuhakikisha wanalipa vinginevyo atawachukulia hatua kali, anaandika, Jovina Patrick.

Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kushtukiza akiwa ameambatana na Kamati ya Uongozi na Fedha ya Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza na wafanyabiashara hao, Mwita amesema kuwa wasipolipa kodi hiyo ifikapo Agosti hatua kali juu dhidi yao zitachukuliwa kwani baadhi yao kuna wadaiwa sugu.

Anasema “Na itakapofika mwezi wa nane nitaagiza wasaidizi wangu na yeyote atakayekuwa hajalipa kodi hatua kali zichukuliwe juu yake”.

Meya amewaonya wafanyabiashara hao juu ya ukaidi wao kutolipa kodi na kusema kuongeza kuwa fedha wanazolipa ni kwa ajili ya manufaa yao wenyewe .

“Pesa hiyo mnayolipa ndiyo inayonunulia umeme, kulipia maji, usafi wa vyoo ni wajibu wenu kulipa kodi,” amesema Meya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!