Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars yabanwa mbavu nyumbani
Michezo

Taifa Stars yabanwa mbavu nyumbani

Wachezaji wa Taifa Stars ikimlinda mchezaji wa Rwanda katika mchezo huo
Spread the love

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kutamba katika uwanja wa nyumbani baada ya kukubali sare ya bao 1-1 dhidi ya Rwanda ‘Amavubi’ katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza, anaandika Erasto Masalu.

Amavubi ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 17 kupitia kwa Domicique Nshuti dakika ya 18 kabla ya Himid Mao kuisawazishia Taifa Stars dakika ya 34 kwa mkwaju wa penalti.

Matokeo hayo yanaipa wakati mgumu Taifa Stars, kwani inatakiwa kushinda katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Jumamosi ijayo jijini Kigali Rwanda.

Taifa Stars ikifanikia kushinda katika mchezo huo wa marudiano itasonga mbele katika hatua nyingine ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika Kenya mwakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!