Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Taifa Stars yabanwa mbavu nyumbani
Michezo

Taifa Stars yabanwa mbavu nyumbani

Wachezaji wa Taifa Stars ikimlinda mchezaji wa Rwanda katika mchezo huo
Spread the love

TIMU ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kutamba katika uwanja wa nyumbani baada ya kukubali sare ya bao 1-1 dhidi ya Rwanda ‘Amavubi’ katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza, anaandika Erasto Masalu.

Amavubi ndiyo ilikuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 17 kupitia kwa Domicique Nshuti dakika ya 18 kabla ya Himid Mao kuisawazishia Taifa Stars dakika ya 34 kwa mkwaju wa penalti.

Matokeo hayo yanaipa wakati mgumu Taifa Stars, kwani inatakiwa kushinda katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Jumamosi ijayo jijini Kigali Rwanda.

Taifa Stars ikifanikia kushinda katika mchezo huo wa marudiano itasonga mbele katika hatua nyingine ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Mataifa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika Kenya mwakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!