Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Channel Ten yawekwa kiporo
Habari Mchanganyiko

Channel Ten yawekwa kiporo

Neville Meena, Katibu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania
Spread the love

JUKWAA la Wahariri Tanzania (TEF) limekiweka kiporo kituo cha Televisheni cha Channel Ten kwa kukiuka makubaliano ya kutoandika wala kutangaza habari zinazomuhusu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, anaandika Hamisi Mguta.

Katibu wa Jukwaa hilo, Neville Meena leo ameeleza kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari amesema TEF inakiri kutangazwa kwa habari za Mkuu wa mkoa huyo zaidi ya mara moja na imekuwa kawaida kwa vyombo vya Sahara Media (Star TV na Radio Free Afrika) kwa kuzingatia kwamba kufanya hivyo ni kukiuka makubaliano na mshikamano wa kitaaluma.

“Uongozi wa Jukwaa unalifanyia kazi hili ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na taasisi husika na baadaye utatoa taarifa rasmi kuhusu matokeo ya mchakato huo, kwasasa tunawakumbusha wahariri na waandishi kwamba makubaliano yetu ya kutotangazwa kwa habari zozote zinazomuhusu Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam bado yapo palepale,” amesema Meena.

Aidha amesema aliyefungiwa kutotangazwa habari zake ni Mkuu wa mkoa na si habari za mkoa  wa Dar es Salaam hivyo habari zinazohusu matatizo, changamoto na maendeleo na maendeleo ya wananchi zinaweza kuandikwa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!