Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ufaransa yakubali kumaliza tofauti na Marekani
Habari Mchanganyiko

Ufaransa yakubali kumaliza tofauti na Marekani

Emmanuel Macron, Rais wa Ufaransa
Spread the love

EMMANUEL Macron, Rais wa Ufaransa ameafiki uamuzi wa Donald Trump, Rais wa Marekani kijitoa katika mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi wa Ufaransa, anaandika Catherine Kayombo.

Macron amesema hayo katika mkutano mjini Paris alipokutana na Trump kuzungumzia tofauti na mitazamo yao kuhusiana na mkataba huo.

“Kuhusu tabia nchi tunajua tofauti yetu, Trump ana ahadi za uchaguzi alizowapatia raia wake na mimi pia nilikuwa na ahadi, lakini vitu hivi havipaswi kuturudisha nyuma ni muhimu kusonga mbele,” alieleza Macron.

Alisisitiza umuhimu wa kuweka makubaliano hayo kando ili viongozi hao watatue masuala mengine muhimu ikiwemo kusitishwa kwa mapigano nchini Syria na Iraq na kuongeza ushirikiano wa kibiashara.

“Marekani inahusishwa zaidi na vita vinavyoendelea nchini Iraq, tumekubaliana kuendeleza juhudi zetu pamoja hususani katika mipango baada ya vita,” aliongeza Macron.

Akizungumza na rais wa Ufaransa, Trump alidokeza kuwa huenda Marekani itabadili msimamo wake hapo baadae, lakini kwa sasa itasimamia uamuzi huo. “Kama mabadiliko yatafanyika itakuwa ni kwa heshima ya makubaliano ya Paris na urafiki kati ya nchi zetu husani katika biashara.”

Trump alijiondoa katika mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi mnamo Juni 2017 katika kutekeleza ahadi aliotoa wakati wa kampeni alipokuwa akigombea urais mwaka 2016. Alidai mkataba huo utahujumu uchumi wa Marekani na kudhoofisha uhuru wa kibiashara katika nchi hiyo.

Aidha uamuzi huo ulipingwa na baadhi ya viongozi wa mataifa 20 makubwa duniani (G20) huku wakiweka ahadi ya kuidhinisha makubaliano ya tabia ya nchi licha ya Marekani kujiondoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

error: Content is protected !!