Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Ufaransa yakubali kumaliza tofauti na Marekani
Habari Mchanganyiko

Ufaransa yakubali kumaliza tofauti na Marekani

Emmanuel Macron, Rais wa Ufaransa
Spread the love

EMMANUEL Macron, Rais wa Ufaransa ameafiki uamuzi wa Donald Trump, Rais wa Marekani kijitoa katika mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi wa Ufaransa, anaandika Catherine Kayombo.

Macron amesema hayo katika mkutano mjini Paris alipokutana na Trump kuzungumzia tofauti na mitazamo yao kuhusiana na mkataba huo.

“Kuhusu tabia nchi tunajua tofauti yetu, Trump ana ahadi za uchaguzi alizowapatia raia wake na mimi pia nilikuwa na ahadi, lakini vitu hivi havipaswi kuturudisha nyuma ni muhimu kusonga mbele,” alieleza Macron.

Alisisitiza umuhimu wa kuweka makubaliano hayo kando ili viongozi hao watatue masuala mengine muhimu ikiwemo kusitishwa kwa mapigano nchini Syria na Iraq na kuongeza ushirikiano wa kibiashara.

“Marekani inahusishwa zaidi na vita vinavyoendelea nchini Iraq, tumekubaliana kuendeleza juhudi zetu pamoja hususani katika mipango baada ya vita,” aliongeza Macron.

Akizungumza na rais wa Ufaransa, Trump alidokeza kuwa huenda Marekani itabadili msimamo wake hapo baadae, lakini kwa sasa itasimamia uamuzi huo. “Kama mabadiliko yatafanyika itakuwa ni kwa heshima ya makubaliano ya Paris na urafiki kati ya nchi zetu husani katika biashara.”

Trump alijiondoa katika mkataba wa mabadiliko ya tabia ya nchi mnamo Juni 2017 katika kutekeleza ahadi aliotoa wakati wa kampeni alipokuwa akigombea urais mwaka 2016. Alidai mkataba huo utahujumu uchumi wa Marekani na kudhoofisha uhuru wa kibiashara katika nchi hiyo.

Aidha uamuzi huo ulipingwa na baadhi ya viongozi wa mataifa 20 makubwa duniani (G20) huku wakiweka ahadi ya kuidhinisha makubaliano ya tabia ya nchi licha ya Marekani kujiondoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!