Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu
Habari Mchanganyiko

TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA
Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekusanya Sh. 9.6 bilioni kutoka kwa kampuni za simu za mkononi kutokana na faini walizotakiwa kulipa baada ya kufanya usajili wa laini za simu bila vitambulisho na kutofuata utaratibu, anaandika Irene Emmanuel.

Kampuni zilizopigwa faini na TCRA kutokana na makosa hayo ya kusajili laini za wateja wa simu bila ya kuwa na vitambulisho na kutofuata utaratibu ni pamoja na Vodacom, Tigo, Zantel, Airtel, Smart na Halotel.

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA, amezitaja kampuni zilizotozwa faini hiyo na kiwango kwenye mabano ni Airtel (Sh1.08 bilioni), Smart (Sh1.3 bilioni), Vodacom (Sh945 milioni), Zantel (Sh105 milioni) na Halotel (Sh1.6 bilioni).

Mkurugenzi huyo amesema hiyo siyo mara ya kwanza kwa kampuni hizo kufanya makosa hayo, na kutolana na kurudia makosa wamepigwa faini nyingine kwa kufanya kosa mara mbili.

Kampuni zilizopigwa faini kutokana na kurudia kosa ni Airtel imetozwa Sh542 milioni, Smart (Sh37 milioni), Tigo (Sh625 milioni), Zantel (Sh52 milioni) na Halotel (Sh822 milioni).

Mhandisi Kilaba amesema kampuni hizo zimetozwa Sh. 500 milioni kila moja kwa kosa la kuathiri na kuhatarisha usalama wa umma na jamii ya Watanzania kwa kusajili laini bila kufuata utaratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!