Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu
Habari Mchanganyiko

TCRA yavuna Sh. 9.6 bil kutoka kampuni za simu

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA
Spread the love

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekusanya Sh. 9.6 bilioni kutoka kwa kampuni za simu za mkononi kutokana na faini walizotakiwa kulipa baada ya kufanya usajili wa laini za simu bila vitambulisho na kutofuata utaratibu, anaandika Irene Emmanuel.

Kampuni zilizopigwa faini na TCRA kutokana na makosa hayo ya kusajili laini za wateja wa simu bila ya kuwa na vitambulisho na kutofuata utaratibu ni pamoja na Vodacom, Tigo, Zantel, Airtel, Smart na Halotel.

Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi wa TCRA, amezitaja kampuni zilizotozwa faini hiyo na kiwango kwenye mabano ni Airtel (Sh1.08 bilioni), Smart (Sh1.3 bilioni), Vodacom (Sh945 milioni), Zantel (Sh105 milioni) na Halotel (Sh1.6 bilioni).

Mkurugenzi huyo amesema hiyo siyo mara ya kwanza kwa kampuni hizo kufanya makosa hayo, na kutolana na kurudia makosa wamepigwa faini nyingine kwa kufanya kosa mara mbili.

Kampuni zilizopigwa faini kutokana na kurudia kosa ni Airtel imetozwa Sh542 milioni, Smart (Sh37 milioni), Tigo (Sh625 milioni), Zantel (Sh52 milioni) na Halotel (Sh822 milioni).

Mhandisi Kilaba amesema kampuni hizo zimetozwa Sh. 500 milioni kila moja kwa kosa la kuathiri na kuhatarisha usalama wa umma na jamii ya Watanzania kwa kusajili laini bila kufuata utaratibu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

Habari Mchanganyiko

Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Greyhorse zasaini mkataba wa bil.7.4

Spread the loveTAASISI ya Mwalimu Nyerere (MNF) imesaini mkataba wa miaka 10...

error: Content is protected !!