Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho
Habari Mchanganyiko

‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho

Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Spread the love

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Foundation For Civil Society (FSC) kesho linatarajia kuzindua kampeni ya “Chungulia Fursa Boda to Bado,” anaandika Victoria Chance.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Boniphace Makene, Afisa Mawasiliano wa shirika hilo, amesema “ lengo la kampeni hii ni kuwahamasisha vijana na wanawake kuzitambua fursa za kibiashara na uchumi zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.”

“Kampeni zitazinduliwa na Balozi Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na tunatarajia kupata washiriki kutoka taasisi 150 ambazo tunafadhili shughuli zao,” amesema Makene.

Makene amesema mbali na kampeni hizo kuzinduliwa jijini Dar es Salaam pia zitaendeshwa katika majiji ya Arusha na Mwanza kwa kuwa ndiyo maeneo makuu ya kibiashara.

“Mafunzo yatakayotolewa kupitia kampeni hii wafanyabiashara wadogo wataongezewa kujiamini na kuwafungua macho kwenye fursa mbalimbali za biashara zinazofanywa katika mipaka ya nchi yetu,” amesema Makene.

Katika kampeni hiyo wamewaalika wafanyabiashara wakubwa kwa lengo la kuwapa changamoto wafanyabiashara wadogo kwa kuwaelezea njia walizopitia mpaka kufikia mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!