Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho
Habari Mchanganyiko

‘Boda to boda’ kuzinduliwa kesho

Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Spread the love

SHIRIKA lisilo la kiserikali la Foundation For Civil Society (FSC) kesho linatarajia kuzindua kampeni ya “Chungulia Fursa Boda to Bado,” anaandika Victoria Chance.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Boniphace Makene, Afisa Mawasiliano wa shirika hilo, amesema “ lengo la kampeni hii ni kuwahamasisha vijana na wanawake kuzitambua fursa za kibiashara na uchumi zilizopo kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki.”

“Kampeni zitazinduliwa na Balozi Dk. Augustine Mahinga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na tunatarajia kupata washiriki kutoka taasisi 150 ambazo tunafadhili shughuli zao,” amesema Makene.

Makene amesema mbali na kampeni hizo kuzinduliwa jijini Dar es Salaam pia zitaendeshwa katika majiji ya Arusha na Mwanza kwa kuwa ndiyo maeneo makuu ya kibiashara.

“Mafunzo yatakayotolewa kupitia kampeni hii wafanyabiashara wadogo wataongezewa kujiamini na kuwafungua macho kwenye fursa mbalimbali za biashara zinazofanywa katika mipaka ya nchi yetu,” amesema Makene.

Katika kampeni hiyo wamewaalika wafanyabiashara wakubwa kwa lengo la kuwapa changamoto wafanyabiashara wadogo kwa kuwaelezea njia walizopitia mpaka kufikia mafanikio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!