Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkude anusurika, mmoja afariki ajalini
Habari MchanganyikoTangulizi

Mkude anusurika, mmoja afariki ajalini

Muonekano wa gari walilopata nalo ajali, Jonas Mkude na wenzake
Spread the love

Nahodha wa Simba, Jonas Mkude amepata ajali mbaya ya gari akiwa njiani kureje Dar es Salaam akitokea Dodoma, anaandika Hamisi Mguta.

Mkude alikuwa akirejea mjini humo baada ya jana Simba kuitwanga Mbao FC kwa mabao 2-1 na kubeba ubingwa wa Kombe la Shirikisho.

Katika gari hilo , lililokuwa na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Landcuiser kupasuka taili na kuanguka.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Shose Fidelis amefariki dunia katika ajali hiyo.

Mkude ni miongoni mwa majeruhi watatu ambapo wawili wamewahishwa katika hospitali ya Morogoro walioambatana na Shose na wenzake kwenda kuishangilia Simba ikipambana kuwania Kombe la Shirikisho.

Shose amekuwa miongoni mwa mashabiki wakubwa wa Simba na amekuwa akionekana pamoja katika lile Kundi la Wapenda Soka ambalo linaundwa na mashabiki wa Simba.

Jonas Mkude

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!