Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mkude anusurika, mmoja afariki ajalini
Habari MchanganyikoTangulizi

Mkude anusurika, mmoja afariki ajalini

Muonekano wa gari walilopata nalo ajali, Jonas Mkude na wenzake
Spread the love

Nahodha wa Simba, Jonas Mkude amepata ajali mbaya ya gari akiwa njiani kureje Dar es Salaam akitokea Dodoma, anaandika Hamisi Mguta.

Mkude alikuwa akirejea mjini humo baada ya jana Simba kuitwanga Mbao FC kwa mabao 2-1 na kubeba ubingwa wa Kombe la Shirikisho.

Katika gari hilo , lililokuwa na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Landcuiser kupasuka taili na kuanguka.

Taarifa za awali zinaeleza kuwa mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Shose Fidelis amefariki dunia katika ajali hiyo.

Mkude ni miongoni mwa majeruhi watatu ambapo wawili wamewahishwa katika hospitali ya Morogoro walioambatana na Shose na wenzake kwenda kuishangilia Simba ikipambana kuwania Kombe la Shirikisho.

Shose amekuwa miongoni mwa mashabiki wakubwa wa Simba na amekuwa akionekana pamoja katika lile Kundi la Wapenda Soka ambalo linaundwa na mashabiki wa Simba.

Jonas Mkude

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!