Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Serengeti Boys kutinga Bungeni Kesho
Michezo

Serengeti Boys kutinga Bungeni Kesho

Kikosi cha timu ya Taifa ya vijana chini umri wa miaka 17, Serengeti Boys
Spread the love

Timu ya Taifa ya Vijana chini ya Umri wa Miaka 17, ‘Serengeti Boys’ ikiongozwa na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) Jamal Malinzi imeondoka leo kuelekea bungeni Dodoma, baada ya kupata mwaliko kutoka kwa Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Serengeti boys imepata mualiko huo baada ya kufanikiwa kufuzu kwenye fainali za kombe la mataifa Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17, ambazo zinatarajia kuanza Mei 21, mwaka huu nchini Gabon.

Timu hiyo ambayo inatarajia kuweka kambi ya mwezi mmoja nje ya nchi kabla ya kuelekea Gaboni, ili kuweza kupata muda mrefu wa maandalizi licha ya kukabiliwa na changamoto kubwa ya kifedha kwa sasa kutokana na timu hiyo ya Vijana kutokuwa na mdhamini kwa sasa.

Licha ya Serengeti boys kuitikia wito huo na kuhudhulia baadhi ya vikao vya bunge vinavyoendelea huko Dodoma kesho, lakini timu hiyo hapo awali ilipokea barua ya pongezi kutoka kwa Spika wa Bunge baada ya kufanikiwa kucheza michuano.

Wajumbe wengine waliongozana na Vijana hao kwenda Bungeni Dodoma, ni Ayoub Nyenzi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu kwa vijana, Mulamu Ng’ambi Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dodoma (DOREFA), Salum Madadi, Alfred Lucas Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Kim Poulsen amabaye ni Mshauri wa Ufundi wa Soka la Vijana na wengine ni .Mwarami Mohammed na Edward Venance.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!