Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani
Habari za Siasa

Lissu agoma kula, ashinikiza kupelekwa mahakamani

Wakili Peter KIbatala (kushoto) akijadili jambo na mteja wake, Tundu Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, amegoma kula chakula kutwa nzima ya leo, akishinikiza kupeleka mahakamani, anaandika Faki Sosi.

Kwa mujibu wa wakili wa Lissu, Peter Kibatala, mteja wake amegoma kula toka asubuhi, mchana na jioni kwa madai hata fanya hivyo mpaka atakapopelekwa mahakamani.

“Mke wa Lissu alileta chakula asubuhi, lakini Lissu aligoma kula na kumwambia mkewe asihangaike kwani hatakuka mpaka atakapofikishwa mahakamani,” amesema Kibatala.

Kibatala amesema kwa sasa wanapigania mteja wake apelekwe mahakamani kwani muda wa kisheria kushikiriwa kituoni umemalizika.

Lissu alikamatwa jijini Dodoma nje ya viwanja vya Bunge, Februari 6, 2017 na kuletwa Dar es Salaam katika kituo cha Polisi cha Kati kwa mahojiano, huku kosa lake likidaiwa ni kauli za uchochezi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!