Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Charles Boniface Mkwasa Katibu Mkuu Yanga
Michezo

Charles Boniface Mkwasa Katibu Mkuu Yanga

Aliyekua Kocha Mkuu wa timu ya Taifa 'Taifa Stars' Charles Boniface Mkwasa
Spread the love

ALIYEKUA kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Charles Boniface Mkwasa ametangazwa kuwa katibu mkuu wa klabu ya Yanga, baada ya kumaliza mkataba wake na shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF).

Kabla ya Mkwasa kuwa kocha muu wa timu ya taifa alikuwa kocha mkuu msaidizi wa wa Yanga chini ya Hans Van Plujim ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa benchi la ufundi wa klabu hiyo .

Mkwasa ameenda kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Dr Jonas Tiboroha ambaye aliondoka klabuni hapo na nafasi hiyo ilikuwa imekaimiwa na naibu katibu mkuu Baraka Deusdedit kwa kipindi cha muda mrefu mpaka uteuzi mwengine ulipofanyika leo.

Toka alipokuwa kocha wa timu ya Taifa, tangu Julai mwaka 2015 baada ya kurithi nafasi ya Mholanzi, Mart Nooij na katika kipindi chake aliiongoza timu hiyo katika mechi 13, ikishinda mbili, kufungwa sita na sare tano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!