Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Matokeo kidato cha nne, Shule za serikali hoi
ElimuTangulizi

Matokeo kidato cha nne, Shule za serikali hoi

Katibu Mkuu wa Necta, Dk. Charles Msonde
Spread the love

MATOKEO ya mitihani ya kidato cha nne iliyofanyika mwaka jana (2016) yametolewa leo ambapo shule za serikali zimeendelea kufanya vibaya huku zile za binafsi zikipeta, anaandika mwandishi wetu.

Katika matokeo hayo jumla ya wanafunzi 277,283 ambao ni sawa na asilimia 70.09 waliofanya mitihani hiyo wamefaulu ambapo madaraja yanayohesabika kama ufaulu ni kuanzia daraja la kwanza mpaka la nne.

Miongoni mwa shule kumi zilizoongoza hakuna shuke yoyote inayomilikiwa na serikali. Shule ya Feza Boys imeshika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na St. Francis Girls, Kaizirege Junior na Marian Girls huku Marian Boys ikishika nafasi ya tano.

Matokeo hayo pia yanaonesha kuwa wavulana wamefaulu kwa asilimia 73.26 huku wasichana wakifaulu kwa asilimia 67.06.

Katika hatua nyingine, shule sita kati ya kumi za mwisho zimetoka katika Jiji la Dar es Salaaam.

Shule hizo ni pamoja na; Kitonga, Nyeburu, Mbopo, Somangila, Mbondole na Kidete ambazo ni za serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!