Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Matokeo kidato cha nne, Shule za serikali hoi
ElimuTangulizi

Matokeo kidato cha nne, Shule za serikali hoi

Katibu Mkuu wa Necta, Dk. Charles Msonde
Spread the love

MATOKEO ya mitihani ya kidato cha nne iliyofanyika mwaka jana (2016) yametolewa leo ambapo shule za serikali zimeendelea kufanya vibaya huku zile za binafsi zikipeta, anaandika mwandishi wetu.

Katika matokeo hayo jumla ya wanafunzi 277,283 ambao ni sawa na asilimia 70.09 waliofanya mitihani hiyo wamefaulu ambapo madaraja yanayohesabika kama ufaulu ni kuanzia daraja la kwanza mpaka la nne.

Miongoni mwa shule kumi zilizoongoza hakuna shuke yoyote inayomilikiwa na serikali. Shule ya Feza Boys imeshika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na St. Francis Girls, Kaizirege Junior na Marian Girls huku Marian Boys ikishika nafasi ya tano.

Matokeo hayo pia yanaonesha kuwa wavulana wamefaulu kwa asilimia 73.26 huku wasichana wakifaulu kwa asilimia 67.06.

Katika hatua nyingine, shule sita kati ya kumi za mwisho zimetoka katika Jiji la Dar es Salaaam.

Shule hizo ni pamoja na; Kitonga, Nyeburu, Mbopo, Somangila, Mbondole na Kidete ambazo ni za serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Walimu 5000 Songwe waililia CWT kuwanyima sare

Spread the loveZaidi ya walimu 5000 ambao ni wanachama wa Chama cha...

error: Content is protected !!