Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Timu Maalim’ wasusa mjengo wa ‘Timu Lipumba’
Habari za Siasa

‘Timu Maalim’ wasusa mjengo wa ‘Timu Lipumba’

Wanachama wa CUF wakiwa nje ya Makao Makuu ya chama hicho, Buguruni, Dar es Salaam
Spread the love

SIKU, saa na dakika zinahesabika kwa Timu Maalim Seif Sharif Hamad kufungua ofisi mpya nje ya ile ya Buguruni jijini Dar es Salaam, anaandika Faki Sosi.

Wameamua kuachana na Ofisi Kuu ya chama hicho ambayo kwa sasa inatumiwa na Timu ya Prof. Ibrahim Lipumba, mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Taarifa kutoka ndani ya chama hicho zinaeleza kuwa, Timu Maalim wamefikia uamuzi huo baada ya Timu Lipumba kung’ang’ania kutumia ofisi ya Buguruni huku mgogoro uliopo ukiwa haujapatiwa ufumbuzi.

Ofisi mpya za CUF Timu Maalim zinatarajiwa kuzinduliwa muda wowote kuanzia sasa katika eneo la Magomeni jijini Dar es Salaam.

Mbarara Maharagande, Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mahusiano ya Umma amethibitisha kuwa, Timu Maalim inatarajia kuzindua ofisi hiyo muda wowote kuanzia sasa ili chama hicho kiendelee na operesheni zake kama kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!