Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Maamuzi ya CAF, Kuhusu rufaa ya TFF
Michezo

Maamuzi ya CAF, Kuhusu rufaa ya TFF

Langa Lesse Bercy mchezaji a timu ya Taifa ya Kongo chini ya miaka 17
Spread the love

BAADA ya sintofahamu ya muda mrefu juu ya rufaa ya Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) juu ya mchezaji wa timu ya taifa ya Jamuhuri ya Congo chini ya umri wa mika 17,Langa Lesse Bercy kutaka kujiridhisha kuhusu umri wake hatimaye kamati tendaji ya Shirikisho la mpira wa miguu Afrika CAF, limetoa nafasi ya mwisho kwa chama cha soka nchini Congo (FECOFOOT) kumpeleka kijana huyo Gabon kwa ajiri ya kipimo cha MRI, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Congo ilifuzu michuano hiyo baada ya kuitoa timu ta taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Tanzania, baada ya kuifunga bao moja kwa bila katika mchezo wa marudiano uliofabyika Kinshasa licha ya Tanzania kushinda katika mchezo wa kwanza kwa mabao 2-1 jijini Dar es Salaam.

Katika taarifa iliyotumwa na CAF katika shirikisho la soka nchini Congo, iliwataka kumpeleka mchezaji huyo ndani ya siku 10 kuanzia Januari 12, 2017 kwa ajiri ya kufanyiwa vipimo ili kujilidhisha juu ya umri wake kabla ya kuanza kwa michuano hiyo.

Hii itakuwa mara ya tatu kwa CAF kumuita mchezaji huyo baada ya mara zote mbili kutokwenda kutokana na sababu mbali mbali wanazozijua shirikisho la mpira wa miguu nchini Congo.

Kwa mujibu wa kanuni za michuano ya kimataifa ya vijana wenye umri wa miaka 17, vijana wanaohitajika kucheza ni wale walio chini ya umri huo wa miaka 17.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!