Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Michezo Azam FC yatwaa ubingwa bila nyavu zake kutikiswa
Michezo

Azam FC yatwaa ubingwa bila nyavu zake kutikiswa

Wachezaji wa Azam Fc wakishangilia ubingwa wa kombe la mapinduzi
Spread the love

BAADA Ya kuifunga klabu ya Simba na kuchukua ubingwa wa kombe la Mapinduzi kwa mara ya tatu, rekodi pekee iliyowekwa na klabu ya Azam Fc katika michuano hiyo ya mwaka huu ni kucheza jumla ya michezo mitano bila kufungwa wala kuruhusu goli lolote, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Goli pekee la Azam Fc katika fainali iliyopigwa jana lilifungwa na kiungo mkabaji Himid Mao kwa shiti la umbali wa mita 25, na kuipa klabu hiyo taji la tatu la michuano hiyo ya Mapinduzi inayofanyika kila mwaka visiwani Zanzibar.

Katika michuano hiyo Azam Fc ilicheza michezo yote bila kuruhusu goli hata moja, mchezo wa kwanza Azam Fc, ilicheza na timu ya  Zima moto na kuibuka na ushindi wa bao moja kwa bila na kwenda sare katika mchezo wa pili dhidi ya Jamhuri na baadae kuipa kipigo kikari Yanga cha mabao 4-0 na kufanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali na kupata ushindi wa bao moja mbele ya Taifa Jang’ombe na baadae kucheza fainali dhidi ya Simba.

Azam Fc ambayo katika michuano hiyo iliongozwa na kocha wake wa muda Iddi Cheche ambaye alikuwa akifundisha timu ya vijana, baada ya kutimua jopo la makocha kutoka nchini Hispania  kutokana na mwenendo mbaya wa timu katika michezo ya ligi kuu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

Michezo

Anza Jumamosi yako na mkwanja wa Meridianbet

Spread the loveJumamosi ya leo ODDS zimekaa kijanja sana ndani ya Meridianbet...

error: Content is protected !!