Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa 240 wauawa Ukraine, 160,000 wakimbia
Kimataifa

240 wauawa Ukraine, 160,000 wakimbia

Spread the love

 

WAKATI vita kati ya Urusi na Ukraine ikiendelea kwa siku ya nne mfululizo, Umoja wa Mataifa umetoa taarifa kuwa hadi sasa jumla ya raia 240 wa Ukraine wamepoteza maisha kutokana na vita hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 27 Februari, 2022 na Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu masuala ya kibinadamu (OCHA) pia imesema jumla ya raia 160,000 wa Ukraine wameikimbia nchi hiyo.

Taarifa hiyo imekuja siku moja baada ya Jeshi la Ukraine kuchapisha kile wanachodai kuwa ni mwanzo wa hasara ya Urusi.

Kulingana na chapisho kwenye ukurasa wake wa Facebook, zaidi ya wanajeshi 3,500 wa Urusi waliohusika katika uvamizi huo wameuawa na karibu 200 kuchukuliwa wafungwa.

Wameongeza kuwa Urusi pia imepoteza ndege 14, helikopta 8, na mizinga 102 hadi sasa.

Rais wa Ukraine, Volodomyr Zelenskky

Hayo yanajiri wakati Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres akirejelea wito wake kwa Rais wa Urusi, Viladmir Putin wa kurejesha majeshi yake nchini Urusi.

Guterres kupitia katika mkutano wake na waandishi wa habari ameeleza hali ilivyo akisema, “tunaona operesheni za kijeshi za Urusi ndani ya eneo huru la Ukraine kwa kiwango ambacho Ulaya haijaona kwa miongo kadhaa. Siku baada ya siku, nimekuwa wazi kwamba hatua hizo za upande mmoja zinapingana moja kwa moja na Mkataba wa Umoja wa Mataifa.

“Wanachama wote wataepuka katika mahusiano yao ya kimataifa kuwa katika tishio au matumizi ya nguvu dhidi ya heshima ya eneo au uhuru wa kisiasa wa nchi yoyote, au kwa njia nyingine yoyote isiyoendana na malengo ya Umoja wa Mataifa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!