Saturday , 11 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wafugaji tuhumani kuwapiga watoto chapa kama mnyama
Habari Mchanganyiko

Wafugaji tuhumani kuwapiga watoto chapa kama mnyama

Spread the love

RIPOTI ya Haki za Binadamu na Biashara imetaja kupungua vitendo vya Ukatili wa kupigwa chapa ya moto kama mnyama kwa watoto mkoani Geita. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Ripoti hiyo iliyoandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binaadamu LHRC imezinduliwa rasmi leo tarehe 16 Agosti 2018.

Akiizungumzia Ripoti hiyo Mkurugenzi wa Kituo hiko Anna Henga amesema kuwa kituo hiko kilibaini matendo ya ukatili dhidi ya watoto kwenye mkoa wa Geita ambapo watoto wenye kutumikishwa kwenye kuchunga mifugo walipigwa chapa ya moto sambasamba na wanyama wanaowachunga.

Ameesema kuwa kituo hiko kilikemea na kutoa elimu kwa jamii ya maeneo hayo ambapo matokeo ya elimu hiyo ni kupungua kwa kiwango kikubwa cha ukatili huo.

Tito Magoti Wakili wa kituo hiko ameleza kuwa LHRC ilipambana kuhakikisha ukatilii huo unakoma kwenye Mkoa wa Geita.

Amesema kuwa utafiti wao ulibaini kuwa hapa nchi vitendo hivyo vipo kwenye jamii ya wafugaji Mkoani Geita ambapo watoto wanatumikishwa kuchunga wanyama kama vile Ng’ombe na Mbuzi nao wanapigwa chapa ya Moto kama wanavyopigwa wanyama hao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!